HII KALI , Wananchi wa Uganda wanapenda kufanya ngono nyakati za mchana hii imedhihirishwa na waziri wa maadili nchini humo.
Baada ya maneno hayo ya waziri huyo wa maadili nchini Uganda kuwa Waganda wengi hujihusisha na vitendo vya kufanya mapenzi hasa wakati wa kipindi cha mlo wa mchana yamezua gumzo kali katika vyombo vya habari nchini humo na katika mitandao ya kijamii.
Simon Lokodo ameongeza kusema wamiliki wa nyumba za kulala wageni wakamatwe kwa kuwaruhusu wafanyi kazi wanaotoka maofisini wakati wa mchana na kwenda kula uroda vyumbani humo.
Wengi wanakiri kuwa tetesi hizo zimeenea nchini humo kwamba wengi wa wafanyakazi hutumia fursa ya mapumziko ya mchana kujihusisha na vitendo vya ngono na makahaba au wapenzi wao wa pembeni.
Baadhi wanaunga mkono kauli hiyo ya waziri lakini wengine wamemtaka asijihusishe na maisha ya wengine.
USIKKOSE KUSIKILIZA MASKANI YA 100.5 TIMESFM KUANZIA SAA 10JIONI KILA SIKU
- Blogger Comment
- Facebook Comment
Subscribe to:
Post Comments
(
Atom
)

0 comments:
Post a Comment