• International News.
  • Fashion News
  • Sports News

ROSE NDAUKA AIBUKA KIDEDEA, ANYAKUA TUZO ZA ZIFF

MSANII wa filamu nchini Rose Ndauka ameibuka kidedea kwa kunyakua tuzo ya msanii bora wa kike huku akiwa amewabwaga baadhi ya wasanii wengine wa filamu akiwemo Lulu, Wema Sepetu, Wolpa, na wengine wengi.

Msanii huyo amenyakuwa tuzo hiyo ya Zanzibar International Film Festival ambapo ni miongoni mwa tamasha la filamu linalifanywa kila mwaka na kuhusisha wasanii mbalimbali kutoka duniani kote.

Akizungumza na mwandishi wa habari hii Ndauka aliweka wazi kuwa filamu iliyomfanya kushinda tuzo hiyo inajulikana kwa jina la 'Waiting Fall' ambayo ilitungwa na yeye mwenyewe pamoja na mpenzi wake.

Alisema kuwa filamu hiyo ndiyo iliyomuwezesha yeye kunyakua tuzo hiyo ikiwa bado ni miongoni mwa ndoto anazozifikiria kuwa msanii wa kimataifa na kujitangaza katika soko la filamu duniani.

Alisema kuwa anawashukuru sana mashabiki zake ambao ndio wamemuwezesha yeye kufikia hapo huku akiweka wazi kuwa bila wao asingeweza kufika katika hatua hiyo ya kuonekana kwa uwezo wake huo wa uigizaji.

Aliweka wazi kuwa tuzo hiyo ni moja ya mafanikio yake ingawa bado anachangamoto kubwa ya kuendelea kupambana katika soko hilo la filamu lililokumbwa changamoto nyingi ili aweze kufikisha malengo yake.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment