• International News.
  • Fashion News
  • Sports News

KAMPUNI ZIKATAZOSITISHA HUDUMA YA MAFUTA KUNYANG'ANYWA LESENI


NAIBU Waziri wa Nishati na Madini Mh. Charles Mwijage ameagiza kampuni yakuuza mafuta nchini kuendelea kutoa huduma hiyo kwa wananchi kwa kuwa serikali inayo hifadhi kubwa ya mafuta.

Naibu Waziri ameyasema hayo leo bungeni jijini Dodoma wakati akitoa ufafanuzi kuhusiana na uwepo wa mgomo katika siku zinazokuja kutokana na kuwepo kwa uhaba wa mafuta ya Petroli na diseli na kusema kuwa serikali itawachukulia hatua wamiliki wa kampuni ya mafuta pale watakapobainika kukiuka na kuvunja sheria.

"Ni kweli na mimi nimeona kwenye mitandao ya kijamii taarifa inayoonesha kukosekana mafuta kwa siku hizi mbili, lakini haiwezi kutokea kwa sababu tunajua kwa takwimu kwamba kwenye hifadhi ya Dar es Salaam, tuna mafuta ya kutosha" alisema

Alisisitiza kuwa wamiliki wa kampuni zinazotoa huduma ya mafuta wasijalibu kuzuia uuzwaji wa mafuta kwani sheria za EURA zinaweza kumfungia mtu yoyote anayezuia mafuta kuuzwa, huku akiweka wazi kuwa leseni ya uuzwaji wa mafuta ni mali ya waziri hivyo wanaweza kuchukua leseni muda wowote kwa yeyote anayekiuka sheria za uuzaji wa mafuta.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment