
Eneo lililokuwa likitumika kuhifadhi mabomba ya kusafirisha gesi toka Mtwara hadi Dar es Salaam ambapo hayo ni baadhi ya malori yaliyokuwa yakisafirisha mambo hayo kama picha inavyoonesha magari hayo yamekwamwa kwenye maji .
Mtu ambaye jina lake halikuweza kufahamika mara moja bila kujali usalama wake, akijaribu kuogelea ili kwend kuokoa tanki la maji (SIMTANK) lililozolewa na maji, hata hivyo mtu huyo hakufanikiwa kwani maji yalikuwa na kasi kubwa (Picha ndogo) akijitahidi kupambana na maji
IMESIBITISHWA kuwa miondombinu ya jiji la
Dar es Salaam imeathirika kwa kiasi kikubwa kutokana na mvua zinazoendelea
kunyesha Tanzania nzima huku huduma ya usafiri ikisimama kwa muda hadi hali ya
miundo mbinu hiyo kutengemaa.
Hayo yalithibitishwa na Kamanda wa kikosi
cha Usalama Barabarani Mohamed Mpinga, ambapo anaeleza kuwa miundo mbinu ya
jiji la Dar es Salaam imeathirika zaidi kutokana kwamba nji eneo la magari
mengi kuingia na kutoka
Akizungumza na tovuti ya Zourhadblog, Mpinga aliweka wazi
kuwa mvua hiyo imeathiri baadhi ya madaraja ikiwemo daraja la Ruvu lililopo
barabara ya Morogoro hali iliyopelekea barabara hiyo kufungwa kwa muda hadi
hapo miundo mbinu itakapokamilika.
Hali hiyo imeibua msongamano mkubwa wa magari na kusababisha safari za wasafiri kukwama kutokana na ubovu wa barabara hiyo iliyosababishwa na mvua inayonyesha.
Wakati huo huo Mpinga anaeleza kuwa
wamezuia magari yanayotoka kituo kikuu cha ubungo, yanayopitia barabara hiyo ya
Morogoro kwenda mikoani ili kuepusha msongamano wa magari wakati barabara hiyo
ikiwa katika matengenezo.
Mpinga ameweka wazi kuwa barabara ya Kilwa pia
imeathirika ambapo daraja lilopo katika
mto Mzinga limekatika hali iliyopelekea pia barabara hiyo kufungwa.
Kutokana na tatizo hilo hali ya usafiri katika
jiji la Dar es Salaam leo imekuwa na msongamano mkubwa kutokana na kufungwa
kwa barabara Morogoro kutokana na daraja lilopo maeneo hayo kuathirika
vibaya.
Pamoja na hayo Kamanda Mpinga ametoa wito kwa wananchi ambao
hawana sababu ya lazima kusafiri kwa kipindi hicho wasitishe safari zao hadi
hapo hali ya mvua itakapotulia na barabara zitakapomalizika kutengenezwa ingawa
kwa sasa hivi juhudi zinaendelea kufanyika.




0 comments:
Post a Comment